Mtemi Fundikira(III)Abdallah Said.(1957-1962).1957-2007 |
Hili ni kaburi la Mtemi Fundikira III, katika Ikulu ya Itetemya. |
Huyu alikuwa Mtemi wa 19 wa Unyanyembe. Utawala wake ulidumu kwa miaka 5 kuanzia mwaka 1957 mpaka 1962. Baada ya Tanganyika kupata uhuru 1961 ndipo Mwalimu Nyerere alipofuta utemi wa dola rasmi mwaka 1962. Mtemi huyu ana historia kubwa sana katika nchi ya Tanganyika pamoja na kuwa haipewi nafasi katika vitabu vya historia na kwingineko. Baada ya hapo alibaki kuwa Mtemi wa jadi tu na asiye na nguvu yeyote ya kuendesha serikali mpaka alipofariki usingizini nyumbani kwake Mwanza Road, Tabora mnamo tarehe 8/8/2007.
Historia zaidi kuhushu Mtemi Fundikira III zitafuata... Hapa akiwa nje ya Ikulu ya Itetemia 1957. |
Ikulu yake iliyopo Itetemia |
Mtemi Fundikira III akitawalishwa 1957 |