Friday, April 15, 2011

Mtemi Fundikira II (Nassor Said) kimala masasi!

Mtemi Fundikira II( Nassor Said)

Dirisha la chumba alichojipigia risasi Mtemi Fundikira III 1957.
Alitawala kuanzia mwaka 1948 mpaka 1957, utawala wake ulidumu kwa miaka 9. Mtemi huyu alipotawala aliweka mikakati ya kukomesha wizi wa mifugo, aliwatangazia wezi wote wajisalimishe kabla hawajatafutwa na kukamatwa, na kweli wezi wote wa mifugo walijisalimisha na wizi wa mifugo hasa ng'ombe ukaisha kabisa katika nchi ya Unyanyembe na jambo hili lilipelekea akatunukiwa medali ya heshima iitwayo ORDER OF THE BRITISH EMPIRE (OBE) na Malkia Elizabeth II katika Ikulu yake Buckingham Palace mjini London. Hii ni heshima kubwa sana ambayo si watanzania wengi wamewahi tunukiwa medali hiyo. Baadae mwaka 1957 ulitokea ubadhirifu wa pesa za serikali katika nchi yake Unyanyembe na ilikuwa dhahiri yeye ndiye kazila, askari wa kikoloni (Waingereza) walipotaka kumkamata akajifungia chumbani mwake na kujipiga risasi na kufa.
Mtemi Fundikira II (Nassor Said) Order of the British Empire.

No comments:

Post a Comment