Thursday, April 14, 2011

Mtemi Mnwasele

Mtemi Isale aka Fundikira kabla ya kufariki alimpendekeza Matandula Mdaki amabye alikuwa ni mpwa wake mtoto wa dada yake Msilu Swetu awe mrithi wake kiti cha utemi. Lakini Mnwasele alipinga Matandula kuwa Mtemi wa Unyanyembe kwa kuwa Matandula Mdaki kwao ni Kigwa na kuna utemi kule, je akifa mtemi wa kwao atatawala nani? au ataenda kutawala yeye tena?  Wazo hilo la Mnwasele wazee waliliunga mkono  na baada ya Mtemi Isale Fundikira kufariki , Mnwasele akaanza kutoa vitisho kwa wazee, kuwa kama wangemtwalisha Matandula Mdaki angemchoma mkuki palepale pa kutawalishia watemi. Basi wazee wakaogopa na kwa kuwa Mnwasele alikuwa shujaa mkubwa katika medani ya vita hivyo wakaamua wamtawalishe yeye na akawa Mtemi wa 10 wa Unyanyembe mnamo mwaka 1859 na utawala wake ulidumu kwa miaka mitano tu.

No comments:

Post a Comment