Thursday, April 14, 2011

Mtemi Kiyungi II

Mtemi Kiyungi alitawala kuanzia mwaka 1864, alikuwa mtoto wa Msagata ndiye aliyezaliwa Uwemba na mama yake alikuwa Muwemba (Zambia) Mara baada ya kutwaa madaraka ya utemi wa Unyanyembe, Mirambo akavamia Unyanyembe zaidi ya mara tano lakini mara hizo zote Mirambo alishindwa vita.


Mtemi  Mirambo
Mtemi Mirambo
 Na kipindi chote cha utawala wake aliandamwa na maneno maneno sana hasa toka upande wa Fundikira uliokuwa ukisema kuwa Kalunde amekosea kumtawalisha Kiyungi  maana hawakua na uhakika kama Kiyungi kweli alikuwa mtoto wa Msagata kweli au vipi! Baada ya maneno hayo kupamba moto, mtoto wa Mtemi Kiyungi aliyeitwa Swetu Kalonga akaenda kumshawishi baba yake kuwa ni bora wawaue kina Fundikira wote ili wao tumbo la Kiyungi waweze kuyawala kwa raha bila shutuma toka tumbo la Fundikira, lakini baba yake alikataa wazo hilo na alimfokea sana Swetu Kalonga na kumwambia "Tena usirudie siku nyingine kunambia maneno kama hayo yaani mimi niwaue bwana zangu walionitoa Uwemba na kunipa kiti cha utawala, wewe una akili kweli wewe? Tena ukome kama ulivyokoma ziwa la mama yako, mimi si mtu mjinga mjinga kama unavyofikiria" Swetu akaondoka lakini akiwa na maamuzi yake kichwani baada ya miezi sita Swetu akaanza kuwaua mwenyewe tumbo la Fundikira. Mtu wa kwanza kumuua alikuwa  Mantumanha na wa pili akawa Kaveve na wengine wengi tu akawaua.Baada ya miaka miwili Mtemi Kiyungi akaamua kumuunga mkono
mwanawe Swetu kuwaua tumbo la Fundikira na akaamrisha Iguli,Msokoni na Kulwa wauawe. Habari hizo zikamfikia Mwanangwa Kalunde binti wa Mtemi Fundikira aliyekuwa akiishi Ndevelwa alikuwa ameolewa na mwarabu mmoja akiitwa  Mohamed bin Hemed el Murjebi huyu ni baba wa Tip Tip. Baada ya Kalunde kupata habari hizo alikasirika sana akapanga kwenda kumtukana Mtemi Kiyungi. Siku ilipofika akaamka saa 11 alfajiri akatoka na walinzi wake na baadhi ya wazee kuelekea Ietemya
akafika pale Itetemya saa 12 asubuhi akamkuta Mtemi Kiyungi ndio kwanza ameamka amekaa katika chake cha utawala akiwa anasubiri watu waende kumsabahi. Kalunde alijifunga nguo tumboni na kuacha maziwa wazi akainua mkono wake wa kushoto na kukinga macho kama anaye kinga jua , akamsogelea Mtemi Kiyungi na kumwambia " wagerahe munuyu mnyaluwemba" Mt Kiyungi akajibu "neneaha mayuu" Kalunde akaanza kumtukana " wewe mnyaluwemba na kupisumbi ulamalawana wansi atiwuli wamuhulaga Mantumana wamuhulaga na Kaveve, Iguli na Msokoni izahangi wamuhulaga Kulwa alumunihuyu Kulwa wasumlakii? Mt Kiyungi akaanguka chini  ya miguu ya Kalunde huku akisema napelage mayuu napelage mayuu napelage mayuu Kalunde akamwambia "ukome kama ulivyokoma kuwaua tumbo la Fundikira kisha kisha akamsonya syoooo akaondoka na kurudi kwake  Ndevelwa. Baada ya hapo Mt Kiyungi akaacha kabisa kuwaua tumbo la Fundikira mpaka alipokufa mwaka 1885.

No comments:

Post a Comment