Mtemi Mirambo |
Mtemi Mirambo |
mwanawe Swetu kuwaua tumbo la Fundikira na akaamrisha Iguli,Msokoni na Kulwa wauawe. Habari hizo zikamfikia Mwanangwa Kalunde binti wa Mtemi Fundikira aliyekuwa akiishi Ndevelwa alikuwa ameolewa na mwarabu mmoja akiitwa Mohamed bin Hemed el Murjebi huyu ni baba wa Tip Tip. Baada ya Kalunde kupata habari hizo alikasirika sana akapanga kwenda kumtukana Mtemi Kiyungi. Siku ilipofika akaamka saa 11 alfajiri akatoka na walinzi wake na baadhi ya wazee kuelekea Ietemya
akafika pale Itetemya saa 12 asubuhi akamkuta Mtemi Kiyungi ndio kwanza ameamka amekaa katika chake cha utawala akiwa anasubiri watu waende kumsabahi. Kalunde alijifunga nguo tumboni na kuacha maziwa wazi akainua mkono wake wa kushoto na kukinga macho kama anaye kinga jua , akamsogelea Mtemi Kiyungi na kumwambia " wagerahe munuyu mnyaluwemba" Mt Kiyungi akajibu "neneaha mayuu" Kalunde akaanza kumtukana " wewe mnyaluwemba na kupisumbi ulamalawana wansi atiwuli wamuhulaga Mantumana wamuhulaga na Kaveve, Iguli na Msokoni izahangi wamuhulaga Kulwa alumunihuyu Kulwa wasumlakii? Mt Kiyungi akaanguka chini ya miguu ya Kalunde huku akisema napelage mayuu napelage mayuu napelage mayuu Kalunde akamwambia "ukome kama ulivyokoma kuwaua tumbo la Fundikira kisha kisha akamsonya syoooo akaondoka na kurudi kwake Ndevelwa. Baada ya hapo Mt Kiyungi akaacha kabisa kuwaua tumbo la Fundikira mpaka alipokufa mwaka 1885.
No comments:
Post a Comment