Friday, April 15, 2011

Mtemi Kalunde Mwana Gumadi

Hili ndilo kaburi la Mtemi Kalunde Mwana Gumadi alitawala 1896-1917


Alitawala baada ya Mtemi Nyamso kufariki mwaka 1896, naye alitawala kuanzia mwaka huo huo mpaka mwaka 1917. Mtemi huyu alikuwa mwadilifu sana na alipenda kusaidia watu kutatua matatizo yao, alikuwa akiamka saa 12 asubuhi na kupita kwenye maofisi kukagua kazi mbali mbali na pia kuona kama maafisa wake wamekwenda maofisini mwao kusikiliza shida za wananchi. Na inapofika mchana chakula kinapokuwa tayari alikuwa akipiga kengele ili mtu yeyote aliyepita hapo aende akale, kwa kifupi alikuwa mtu mkarimu sana. Ilipofika mwaka 1917 alifariki.

No comments:

Post a Comment