Friday, April 15, 2011

Mtemi Saidi Fundikira (Sultan Said)

Hili ndilo kaburi la  Mtemi Swetu(Said) Fundikira alizikwa hapo mwaka 1961.
Mtemi Saidi Fundikira (Sultan Said) huyu alikuwa Mtemi maarufu sana katika nchi ya Tanganyika, alitawala kuanzia mwaka 1917 mpaka 1927. Alifanikiwa kuwashawishi watemi wengine  wa kanda ya magharibi kuchanga pesa, mifugo na mali nyingine ili

Mtemi Said (sultan said) Fundikira 1956
Sultan Said Fundikira na Mw Nyerere 1956

Mzee Ramadhani said Fundikira

kupata pesa za kujenga shule mbili za Tabora Boys na Tabora Girls. Na yeye akatoa ardhi ya kujenga shule hizo kwa kuwa eneo hilo lilikuwa chini ya himaya ya Ikulu ya Unyanyembe. Vile vile Mtemi Said alikuwa mkarimu mno kiasi kwamba mtu akiunguliwa na nyumba yeye alimjengea nyumba mpya na kumpa chakula cha kumtosha kwa mwaka mzima. Na kila mwisho wa mwezi alipokuwa akitoka Bomani kuchukua mshahara wake ulikuwa ni shilingi 4000, ambazo hata Gavana wa Kiingereza Bw Donald Cameron alipata kiasi hicho pia. Watu wenye shida walijpanga katika barabara ya Luhanzali wakimtolea shida zao naye aliwasaidia kwa kuwapa pesa za mshahara wake na hata alipofika Ikulu Itetemia alijikuta kuwa ameishiwa pesa zote.  

Yeye aliondolewa madarakani na wakoloni wa kiingereza baada ya kuwa hapeleki serikalini kodi aliyotoza wananchi, inasadikika alitumia pesa hizo kusaidia masikini. Hivyo kwa heshima na upendo aliyokuwa nao kwa wananchi wake wakoloni wa Kiingereza walilazimika wasimfunge jela ila walimuondosha Itetemia na kiti chake akakitwaa Mtemi Kiyungi II huyu alikuwa mtoto wa Mtemi Isike Mwana Kiyungi. 

Sultan Said alijaaliwa kupata watoto 57 ambao miongoni mwao ndio hawa kina marehemu Chief Abdallah Fundikira, Ramadhani Mlawila (Baba yangu), Kagori biti Said (Mama yake Samuel Sitta) na wengi wengine.Na mpaka sasa katika watoto hao 57 wamebaki wanawake watatu Kagori na Ndisha na mwanamume mmoja Ramadhani Mlawila (87) aliyepata kuwa waziri mkuu katika ofisi ya Mtemi Fundikira III pia aliwahi kukaimu Utemi wakati Mtemi Abdallah (Fundikira III) alipoingia serikalini.

Nyumba hii ilitumiwa na waziri mkuu Mlawila 1957-64

Ninavyofikiri mimi Sultan Said ndiye aliyeuingiza ukoo huu wa Fundikira katika dini ya ki Islam, kwa kuwa yeye alisomea Zanzibar ambako dini hiyo ilishasambaa huko. Bila shaka aliporudi bara ndipo akaja na dini hiyo ambayo mpaka sasa ndiyo imekua dini ya Ukoo huu. Na hakuna ushahidi kama ukoo huu uliwahi kuwa waumini wa dini yeyote kabla miaka ya 1900. Hivyo basi inaelekea ukoo huu uliabudu mizimu kama ilivyo desturi ya wa Afrika.
Sultan Said aliishi katika nyumba hii baada ya kuruhusiwa kurudi Itetemia

4 comments:

  1. Lo, hii historia kweli. Nilikuwa siyajui hayo.

    ReplyDelete
  2. Nimependa historia ya ukarimu wa. Fundikila kwa kutoa ardhi ya kujenga shule

    ReplyDelete
  3. Sawa ila kuna wadogo zenu wanagombania ardhi, vipi wao sio kama babu yao?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Siyo kugombania ni kuisalimisha kutoka kwa wanafamilia wachache wenye tamaa ni hivyo tu.

      Delete